Social Icons

Wednesday, 30 October 2013

MTANZANIA ZINDUKA....






Na: Meshack Maganga-Iringa.

Tunakabidhiwa dhamana kubwa ambayo ingetusaidia sana maishani mwetu, lakini tunacheza nayo hadi inapotea kwa sababu tu hatuamini kwamba utunastahili kuitumia kufika juu. Tunaziona nafasi za kusonga mbele, lakini tunaamini kwamba, hatustahili kuzitumia.

Fursa zikija waziwazi kabisa, tunajifanya hatuzioni kwa kutafuta visingizio mbalimbali ili tusizitumie, kwa sababu tu, tumeamini kwenye mawazo yetu kwamba, sisi hatustahili.
Ni vigumu kugundua kwamba nafasi au fursa hizo zimekuja kwa sababu tayari tumejifungia njia kuelekea mafanikio. Wengine kwa bahati mbaya wanaweza kuona na kubaki wameshangaa ni kwa nini tushindwa kuinuka katika mazingira tuliyomo.

Mtu anapoamini kwamba hawezi, anayaambia mawazo yake ya kina yamsaidie kumfanya ashindwe zaidi kwenye kila jaribio analofanya. Badala ya kufanya juhudi kujisaidia ili amudu, hujipweteka kwa kuamini kwake kwamba hata kama atafanya kitu gani, kamwe hatamudu. Siyo rahisi kwa mtu mwenye mawazo ya aina hii kuweza kufanikiwa maishani.
Kuna watu ambao kwa sababu ya kukosa kile ambacho jamii inakiona kuwa ndiyo ufunguo wa mafanikio, huwa wanaamini kwamba hawawezi kufanikiwa au kufanya vizuri maishani kama hao ambao wanacho. Kwa mfano, kwa kukosa elimu, ujuzi au utaalamu fulani, watu wengine hujihesabu kama wanyonge. Huchukulia kwamba ni wale tu wenye elimu, ujuzi na utaalamu fulani ndiyo wanaoweza au wanaotakiwa kufanikiwa.


Soma zaidi hapa

0 comments:

Post a Comment