Social Icons

Sunday, 7 April 2013

KANUMBA DAY @LEADERS - 7/04/2013......


 
Leo mwaka umepita tangu aliekuwa muigizaji nguli nchini, Steven Charles Kanumba atututoke. Kanumba atakumbukwa kama mmoja ya wasanii waliofanya tasnia ya filamu nchini izidi kukua na kupendwa hadi kuteka soko ambalo kwa kiasi kikubwa lilikuwa likishikiliwa na wasanii wa Nigeria. Aliondoka wakati bado hajayafaidi mafanikio na kushuhudia namna mapinduzi aliyofanya yalivyotengeneza ajira kwa vijana wengi.

Pumzika kwa amani The Great Steven Kanumba.
 
 
Familia ya Kanumba inawakaribisha katika kumbukumbu ya mwaka mmoja ya kifo cha marehemu Kanumba itakayofanyika Leaders Club siku ya jumapili hii tarehe 7/4/2013 kuanzia saa 8 mchana.Kutakuwa na uzinduzi wa muvi ya mwisho kufanywa na marehemu. Pia itaoneshwa kwa mara ya kwanza preview ya movie iitwayo After death(Never happened before) iliyoandaliwa na Jackline Wolper kwa ajili ya kumuenzi marehemu Kanumba.
Kutasindikizwa na Twanga Pepeta na wachekeshaji maarufu Tanzania.
 
 
 

KIINGILIO NI BURE. MSIKOSE TUMUENZI NDUGU YETU.


0 comments:

Post a Comment